• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZAZI TIMIZENI WAJIBU WA KUWALEA WATOTO WENU -RC MTANDA

Posted on: April 14th, 2025

WAZAZI TIMIZENI WAJIBU  WA KUWALEA WATOTO WENU -RC MTANDA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Aprili 14,2025 amezindua rasmi mkakati wa kutokomeza watoto wa mitaani na kutoa rai kwa wazazi kutimiza wajibu wao wa malezi.

Akizungumza na makundi mbalimbali yanayojihusisha na malezi kwa watoto na watoto wa mitaani kwenye ukumbi wa Ofisi yake Mtanda amesema chanzo cha kuwepo kwa watoto mitaani ni wazazi kushindwa kutimiza majukumu yao ya ulinzi na malezi bora kwa watoto wao.

"Nichukue nafasi hii leo kuhimiza hili jambo, ile adhabu ya kulipa Tshs. Milioni 5 au kifungo cha miezi sita jela ipo palepale kwa wale wazazi watakaobainika kwenda kinyume cha sheria nawasihi wadau mliopo hapa tushikamane kutoa elimu kwa jamii",Mkuu wa Mkoa.

Aidha amebainisha migogoro ndani ya familia,umasikini,pamoja na kutoandikwa mirathi nayo imechangia kuwepo kwa ongezeko la watoto wa mitaani.

Ameyapongeza pia mashirika yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na watoto wa mitaani kwa kujisajili rasmi na kufanya shughuli zao kwa kuzingatia miongozo iliyopo.

"Asilimia 70 ya mashirika yasiyo ya kiserikali mkoani Mwanza yalikosa sifa za kufanya shughuli hizi lakini sasa karibu yote yapo rasmi na tunaendelea kushirikiana nayo kupambana na hali hii.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jessica Lebba amesema Mkoa wa Mwanza ni wa pili kwa idadi kubwa ya watoto wa mitaani lakini wamejipanga kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Ofisi yake,fawati la ukatili wa kijinsia kuhakikisha elimu ya kuzingatia ulinzi na usalama wa mtoto inatolewa kwa jamii.

"Uzinduzi huu wa leo Mkoa wa Mwanza unakuwa  wa kwanza kufanya hivyo hapa nchini,hii ni kuonesha tulivyodhamiria kupambana na hatimaye kutokomeza watoto wa mitaani",Lebba


Mmiliki wa kituo cha DayCare Linah Roman amesema jukumu walilonao hivi sasa ni kuhakikisha wanashirikiana na Serikali kutokomeza hali ya umasikini ndani ya jamii.

Uzinduzi huo uliohudhuriwa na Maafisa ustawi wa jamii kutoka wilaya za Nyamagana na Ilemela ulikwenda pamoja na ugawaji wa vyeti vya kuwatambua kwa baadhi ya vituo vya kulea watoto.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.