• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WATUMISHI RS MWANZA WAPIGWA MSASA ELIMU YA BIMA

Posted on: March 3rd, 2025

WATUMISHI RS MWANZA WAPIGWA MSASA ELIMU YA BIMA


Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeendesha kikao cha utoaji elimu ya Bima kwa Watumishi wa Serikali kuhusu uhamasishaji wa matumizi ya bidhaa za bima.

Akifungua kikao hicho mapema leo Machi 03, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ametoa rai kwa Watumishi hao kuhakikisha wanakuwa makini katika kusikiliza elimu hiyo ili ikawe na manufaa kwao na kwa wale ambao hawajahudhuria.

Katibu Tawala amesema ni matarajio yake kuwa elimu hiyo itawasaidia na kuhakikisha wanakuwa mabalozi wa bima kwa jamii wanayoihudumia, na kusaidia katika urahisishaji wa upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi.

Aidha Bw. Balandya amesema kutokana na Sheria ya bima ya afya kwa wote ametumia jukwaa hilo pia kuwataka Watumishi na wadau kwenda kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu na faida za bima ili wananchi waweze kujitokeza kwa wingi katika kukata bima.

“Uelewa wa elimu ya bima ni msingi wa mafanikio ya utekelezaji wa bima ya afya kwa wote, niwatake muwe makini katika kusikiliza na kuelewa”.

Naye Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware ametoa rai kwa watumishi wa Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kuwa mali na miradi mikubwa ya Serikali inakatiwa bima ili kupunguza hasara zinazoweza kutokea wakati wa majanga.

Aidha amesmea bima haimkingi mtu tu bali majanga mbalimbalo ambapo kwa sasa hata wale wakulima, wafugaji na wajasiriamali wadogo wadogo nao wanaweza kukinga bidhaa, mazao na mali zao.

“Bima za Kilimo, mifugo zipo lakini tunakosa watu kwa sababu hawana uelewa wa kutosha, elimu hawana, niwaombe mkatufikishie elimu hii ili waweze kukata bima hizo”.

TIRA wako Mkoani Mwanza wakilenga kuwaelimisha Watumishi kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya bima, ikiwa ni pamoja na kuwa mawakala wa bima na utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.