• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AIPONGEZA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KUENDELEA KUFIKIKA

Posted on: March 3rd, 2025

RC MTANDA AIPONGEZA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KUENDELEA KUFIKIKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa pongezi kwa Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuendelea kuwafikia wananchi kwa ukaribu zaidi na kutatua changamoto zao pamoja na utoaji wa elimu kuhusu masuala ya sheria.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo mapema leo Machi 03, 2025 wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya Wajumbe wa Kamati ya Usalama Mkoa kuhusu Elimu ya Uraia na Utawala Bora ambapo yamewakutanisha Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati za Usalama za Wilaya, baadhi ya Wataalam wa Halmashauri na Watendaji wa Kata zote za Mkoa wa Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema uchangamanaji wa Wizara hiyo na Wananchi umekuwa na tija kubwa kwa jamii kwani imekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wenye changamoto mbalimbali za kisheria ambapo wamekuwa wakipatiwa ufumbuzi.

kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) iliyozinduliwa tarehe 18 Februari, 2025 hapa Mkoani Mwanza lakini pia Kamati ya msaada wa kisheria na leo mafunzo haya, yote haya yanaifanya Wizara hii kuendelea kuonekana.

“Hatua hii imesaidia Serikali kuendelea kuaminiwa na Wananchi, kuimarisha amani na mshikamano ndani ya jamii”.

Kadhalika ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuona umuhimu wa kuendesha mafunzo hayo na ni wazi kuwa mafunzo hayo yataongeza uelewa na tija kuhusu masuala ya Uraia na Utawala Bora.

“Ninafahamu kuwa wote tunaoshiriki mafunzo haya tunawawakilisha viongozi walio chini yetu na ni imani yangu kuwa mafunzo haya yatatusaidia kuongoza kwa kuzingatia misingi ya Utawala Bora”.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji Haki,  Bw. Lawrence Kabigi amesema Mafunzo hayo ya elimu ya uraia na Utawala bora yanayowalenga viongozi kuanzia ngazi ya Mkoa, Wilaya hadi Halmashauri yana lengo la kuwajengea uwezo viongozi na wataalamu kufanya kazi kwa kuzingatia sheria za nchi

“Wizara ya Katiba na Sheria imekuwa kinara wa kutumia 4R za Mhe. Rais yaani Maridhiano, Ustahimilivu, Mabadiliko, na Kujenga upya ili kuwepo na Utawala bora na wananchi kuishi kwa amani na upendo miongoni mwao”.

Mafunzo ya Elimu ya Uraia na Utawala Bora hadi sasa yameshafanyika kwenye mikoa kumi na moja (11) kwa kuwatumia watoa mada kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Tawala za Miko na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jeshi la Polisi na Tume ya haki za binadamu na Utawala bora, Na kwa sasa mafunzo hayo yanaendelea kutolewa kwenye mikoa sita (6) ukiwemo Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.