• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

Posted on: April 29th, 2025

MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA


Itakumbukwa mnamo machi 16 na machi 26, 2025 Makundi mawili ya Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza walikwenda kufanya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Ngorongoro, Hifadhi ya Taifa ya Mwl. Nyerere, Mradi wa kimkakati wa kufua umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) na Mradi wa reli ya kisasa kutoka Mkoa wa Dar es Salaam kwenda Dodoma.

Leo Aprili 29, 2025 makundi hayo mawili kwa uwakilishi yamewasilisha neno la shukrani na zawadi kadhaa Ofisini kwa Mratibu na Muasisi wa Ziara hizo ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana.

Akizungumza ofisini kwa Katibu Tawala, Kiongozi wa Kundi la JNHPP Bw. Paulo Cheyo amesema ilikua ni wasaa mzuri sana kutembelea mradi wa kimkakati wa JNHPP na wameweza kujifunza mengi na kumtakia kila la kheri KIongozi huyo mwenye maono mema kwa Watumishi wake.

“Hakika safari yetu ilikua nzuri na yenye mafunzo, Binafsi sikuwahi kufikiria kufika kutazama uwekezaji mkubwa uliofanywa katika bwawa la Mwl. Nyerere, Ninakushuru sana Kiongozi kwa jitihada zako”. Amesema Bw. Mangabe Mnilago.

Naye Kiongozi wa Kundi la Ngorongoro - Serengeti Bw. Credo Lugaila amesema ziara hizo pia zimesaidia kuwachangamsha na kuleta ari ya ufanyaji kazi, lakini pia amesema imesaidia kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Watumishi na Viongozi wa Mkoa.

“Maneno Matakatifu ya Biblia yanasema upendo wa ndugu na udumu, Tunakushuru sana Baba kwa upendo wako, umethibitisha maana halisi ya Kiongozi anaejali na kuwathamini Watumishi wake, Tunakushuru sana. Amesema Bi. Ine Sibale

Akihitimisha kutoa shukrani hizo Bi. Zawadi Kalilo amesema upendo wa Katibu Tawala ni kama upendo wa Baba lakini kwa Kiongozi huyo kwa Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amekuwa kama “Daddy”. (Akimaanisha mwenye upendo uliokithiri).

Akizungumza mara baada ya kupokea salamu hizo, Katibu Tawala Bw. Balandya Elikana amewashukuru kwa maneno mazuri ya faraja pamoja na maombi na amewataka sasa kwenda kuchapa kazi kwa ufanisi na weledi.

Makundi hayo mawili yamewawakilisha wale Watumishi waliopata wasaa wa kufanya utalii na wamemzawadia kiongozi huyo zawadi mbalimbali ikiwa ni kitambua mchango wake katika kuwathamini Watumishi hao na kwake ikawe kumbukumbu halisi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.