• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA Yatoa elimu kwa Wadau wa Huduma za Mawasiliano

Posted on: April 4th, 2019

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania  imefanya Mkutano na wadau  wa huduma za mawasiliano  Mkoa wa Mwanza  ikiwa na lengo la kukumbushana taswira ya Sheria ya Makosa ya Mitandaoni ya mwaka 2015,Matumizi bora ya mitandao ya kijamii,changamoto za watumiaji wa mawasiliano na kuelimisha Umma na utatuzi wa malalamiko hayo.

Akiongea katika kikao hicho Mkuu wa Kanda ya Ziwa Mamlaka ya Mawasiliano Mhandisi Fransis Mihayo amesema kutokana na ukuaji wa tekinolojia kumekuwa na uelewa mdogo wa watumiaji wa mitandao hivyo kifanya makosa ya kimitandao kuongezeka kila siku.

" Mamlaka inayo orodha ya watoa huduma mitandaoni wanaoendelea kurusha maudhui kwa kuvizia, inawataadharisha kuacha kuvunja sheria, bali wafuate taratibu za usajili,"alisema Mhandisi Mihayo.

Aidha amewaomba viongozi wa dini wakati wakiendelea kutujenga na kutuimarisha kiroho, watukumbushe pia uwepo wa changamoto ya matapeli mitandaoni na kamwe kila mtu hapaswi kutoa ushirikiano wa aina yoyote kwa kujibu ujumbe mfupi na kuendelea na mazungumzo na matapeli kupitia simu.

Naye Kamishna Msaidizi wa polisi Muliro J.MULIRO amesema maendeleo makubwa  ya kitekinolojia yameleta ongezeko kubwa la huduma mbalimbali mitandaoni, na kuleta msukumo mkubwa wa ukuaji katika Sekta ya mawasiliano.

"Mwaka 2000 kulikuwa na laini za simu 284,109 idadi hii imeongezeka hadi laini milioni 43 kwa sasa wakati huduma za intaneti wameongezeka  kutoka milioni 3 na laki tano kwa miaka 5 iliyopita hadi milioni 17 hivi leo," alisema Kamishna Muliro.

Kwa upande wao watoa huduma kutoka Vodacom wakiwakilishwa Mkuu wa Kanda ya Ziwa Victoria, Ayubu Kalutya  amesema wao hufanya kazi hadi jumamoai hivyo wangependa hata Jeshi la polisi lingefanya hivyo hasa wanaohuaika na taarifa ya upotevu 'loss report' kwani wateja huchukua muda mrefu kupata taarifa hii, pia huwachelewesha kurudisha line zao.

"Kuwe na udhibiti wa simu ili makampuni yanayotoa huduma za simu yaweze kuendesha huduma kuwezs kuwa na mawasiliano mazuri na wateja wao,"alisema Kalutya.

Aidha Mkuu Msaidizi wa Kitengo cha uhalifu wa kimtandao kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, ASP Joshua Mwangasa amesema, kuna changamoto kubwa ya kutoa taarifa za uongo hivyo jeshi la polisi linakabiliana na kila mvunjifu wa kosa hilo, hata hivyo ushirikiano mkubwa kati ya Jeshi la polisi na wananchi inasaidia kuleta amani.

"Ili kuepuka kufanya makosa ya mtandao  ni vema kufuata sheria,kuwa na hofu ya mungu, kuepuka kutuma taarifa udiyo na uhakika nayo na kuhakikisha kila mtu anatoa taarifa kwa jeshi la polisi pale ualifu unapotokea,"alisema ASP Mwangasa.

Aidha, ushirikiano unatakiwa ili kuleta amani kwani baadhi ya mitandao ya kijamii ipo nje ya nchi hivyo Mamlaka ya Mawasiliano haina mamlaka nayo.

Hata hivyo amesisitiza kuwa uvunjifu wote wa sheria uripotiwe polisi ili wahalifu wakabiliwe na sheria ifuate mkondo wake, pia ulinzi uanzie kwa mtu mwenyewe.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA MWANZA MWAKA 2021 December 18, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2018 Shule za Sekondari za Serikali Mkoa wa Mwanza December 13, 2017
  • Ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji katika shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mwanza 2018 January 10, 2018
  • Ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA Kitaifa Mkoa wa Mwanza. June 07, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AGA KHAN Yatoa Vifaa vya Bilioni 1.5 Kuepusha vifo vya mama na mtoto Mwanza

    December 22, 2020
  • Kikao cha bodi ya Barbara chapanga mikakati ya mafanikio Mwanza

    December 21, 2020
  • Mwanza Kwanza Toleo la pili kwa habari mbalimbali Mkoa wa Mwanza

    December 12, 2020
  • Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

    December 10, 2020
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella akifungua Baraza la biashara katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkikutano uliopo katika ofisi ya Mkoa uliojumuisha wajumbe mbalimbali wa Baraza hilo wa Mkoa wa Mwanza.
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Regional Drive Mkabala na Ofisi za TRA

    S.L.P: S.L.P. 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.