MAELEZO YA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2008/2009 KATIKA SEKRETARIAT YA MKOA NA HALMASHAURI ZA WILAYA NA JIJI Ili mkoa uweze kutekeleza miradi mbalimbali iliyojipangia mkoa unaomba kuidhinishiwa fedha za maendeleo kama ifuatavyo:-
1. Mradi Na.6340 UPANUZI WA OFISI YA MKUU WA MKOA
Mkoa umeidhinishiwa Tshs. 367,764,000 katika Kitengo cha Utawala ili kiweze kupanua Jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kulikarabati kutokana paa lake kuchakaa sana na baadhi ya ofisi za wafanyakazi. Kama nilivyoeleza katika sehemu ya mapitio ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya mwaka 2007/2008, jengo hili bado linahitaji upanuzi/ukarabati mkubwa kama vile, kuezeka paa kwa kutumia vigae, kukarabati ofisi za wafayakazi na kupaka rangi uzio wa jengo. Kutokana na ufinyu wa bajeti shughuli ya ujenzi wa jengo haujakamilika ipasavyo. Mradi huu si mpya umeanza kutekelezwa miaka miwili iliyopita. Kati ya fedha zinazoombwa katika mradi ni kwa ajili ya upanuzi wa jengo.
2. Mradi Na. 6339 UKARABATI WA NYUMBA YA RAS
Mkoa umeidhinishiwa Tshs. 45,000,000 kwa kukarabati nyumba ya RAS. Kama nilivyosema katika miradi mingine ya kukarabati majengo ya serikali, nyumba hii ilijengwa wakati wa ukoloni na kuta zake, paa, madirisha na milango inahitaji kukarabatiwa. Kutokana na ufinyu wa bajeti mradi huu ulipangwa kufanyika kwa awamu. Mradi huu vile vile si mpya ulianza mwaka juzi
3. Mradi Code No. 6348 UKARABATI WA NYUMBA YA RCMkoa umeidhinishiwa Tshs. 50,000,000 Katika Kitengo cha Utawala ili kiweze kukarabati nyumba ya Mkuu wa Mkoa ambayo paa lake limechakaa na servant quarter kuharibika sana. Katika mwaka 2008/2009 mkoa umepanga kukarabati nyumba ya RC kwa kuezeka paa jipya, kuendelea kukarabati sakafu ya jengo, kukarabati madirisha na milango, kuweka mfumo mzuri wa maji safi na taka. Kutokana na ufinyu wa bajeti ukarabati huu pia unafanyika kwa awamu. Mradi huu ulianza kutengewa fedha mwaka wa fedha 2003/2004.
4.Mradi Na.6337 UJENZI WA OFISI ZA WAKUU WA WILAYA
Mkoa umeidhinishiwa Tshs. 340,000,000katika Kitengo cha Utawala ili kiweze kujenga Ofisi za Wakuu wa Wilaya ya Ilemela na Nyamagana ambao kwa sasa hawana ofisi na wanapanga kwenye majengo ya watu binafsi au Taasisi, majengo ambayo hayana hadhi ya kuwa ofisi za Serikali. Katika mwaka 2007/2008 mkoa umepanga kumaliza kabisa ujenzi wa ofisi hii ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela kwa kuitengea Tshs…85,000,000 na zinazobaki Tshs. 255,000,000 zitatumika kuendeleza ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana ambaye hana ofisi na anapanga katika jengo la H/Jiji.
5. Mradi Na. 6532 MFUKO WA MKUU WA MKOA WA UCHANGIAJI KATIKA MIRADI YA KUJITEGEMEA.
Mkoa umeidhinishiwa Tshs. 20,000,000 Katika Kitengo cha Utawala ili kumuwezesha Mkuu wa Mkoa kuchangia katika miradi ya kujitegemea inayoanzishwa kwa nguvu za wananchi wenyewe. Kama nilivyosema mwanzo fedha za mradi huu zinamuwezesha Mkuu wa Mkoa kuchangia katika miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na wananchi na vikundi vilivyoanzisha na kutekeleza miradi yao. Lengo la Mkuu wa Mkoa kutengewa fedha hizi ni kutaka kumfanya awaongezee ari na hamasa wananchi katika kujiletea maendeleo. Katika mwaka 2008/2009 jumla ya miradi 50 inakadiriwa kuchangiwa. Miradii hii itakuwa katika sekta ya ujenzi wa shule za sekondari, ujenzi wa madarasa ya shule za msingi, vyama vya akiba na mikopo (SACCOs), watoto yatima na vikundi vya akina mama na vijana na watoto yatima na walemavu.
6. Mradi Na. 6531 USHIRIKISHWAJI JAMII
Mkoa unaomba kuidhinishiwa Tshs 5,000,000 Katika Kitengo cha Mipango na uratibu ili kuwezesha wataalam wafuatilie utekelezaji wa O & OD Participatory Planning huko wilayani. Lengo la mradi huu ni kufuatilia ufahamu na utekelezaji wa O & OD participatory appraisal. Mradi huu ulianza mwaka juzi kufuatilia utekelezaji wa mipango shirikishi.
7. Mradi Na. 4404 USIMAMIZI WA PROGRAMU YA DADPS
Katika kitengo cha Economic Development Support Services Mkoa unakiombea Tshs 5,700,000 ili kuwezesha wataalam wa Kitengo kufuatilia utekelezaji wa miradi ya District Agricultural Development Programme DADPS inayotekelezwa na Halmashauri. Katika mwaka 2008/2009 mkoa utatembelea Halmashauri zote na kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi na kutoa ushauri kwa Halmashauri juu ya utekelezaji wa mradi. Mradi huu si mpya ulianza mwaka wa fedha wa 2006/2007.
8. Mradi Na. 6239 UPANUZI WA HOSPITALI YA MKOA
Mkoa unakiombea Kitengo cha Curative Services kiasi cha Tshs. 600,000,000 Ili kiweze kuendelea kuipanua hospitali ya mkoa ambayo ni muhimu sana kwa huduma za afya kwa wananchi wa mkoa wa Mwanza. Katika mwaka 2008/2009 mkoa utaendelea na mpango wake wa upanuzi wa hospitali kwa kukarabati baadhi ya maward na sehemu ya mapokezi. Pia utachagia katika mradi wa UKIMWI ulioanzishwa hapa hospitalini.
KIFUNGU Na. 8091 Ruzuku kwa Miradi ya Maendeleo ya Halmashauri za Wilaya na Miji Tshs. 26,989,764,000
9. Mradi Code No. 6401
Mkoa unaziombea Halmashauri za Wilaya Tshs. 22,462,835,000 ili ziweze kutekeleza Miradi ya Maendeleo walinayojiwekea kwenye mipango yao iliyopitishwa na Mabaraza yao ya Madiwani. Kati ya fedha hizo Tshs 2,856,825,000. zitatolewa na serikali Kuu na Tshs 19,606,010,000 ni fedha za nje.
10. Mradi Code No. 6402 Mkoa unaiombea Halmashauri ya Jiji la Mwanza Tshs. 4,526,929,000. Ili liweze kutekeleza Miradi ya Maendeleo walinayonayo kwenye mipango yao iliyopitishwa na Madiwani wao. Kati ya fedha hizo Tshs 170,647,000 zitatolewa na Serikali Kuu na Tshs 4,356,282,000 itatolewa na wafadhili mbalimbali.
11. Mradi code 6339 Mkoa unaomb jumla ya Tshs 85,000,000 kuanza ujenzi wa nyumba ya DAS wa Wilaya ya Ukerewe katika mwaka wa fedha 2008/2009. Nyumba ya DAS ilijengwa kwa kutumia udongo wa tope hivyo haiwezi kukarabtika kutokana na uchakavu mmkubwa wa nyumba hiyo. |