JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
 
     
SEKTA YA MIPANGO :
 
[ Mipango ] [ Nyumbani ] au
 

Idara ya Mipango ina majukumu ya Kuratibu, kufuatilia na kutoa huduma katika nyanja mbalimbali, yafuatayo ni majukumu ya Idara hii:

  1. Kuratibu masuala yote ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
  2. Kuratibu Mipango na Bajeti ikiwemo Mpango Mkakati na Mipango kazi.
  3. Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa mkataba wa huduma kwa wateja.
  4. Sekretarieti katika vikao vya Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC).
  5. Kuunganisha, kuratibu na kufuatilia Mipango na Bajeti za Serikali za mitaa.
  6. Kutoa huduma za kitaalam katika utekelezaji wa Mfumo wa habari na mawasiliano.
  7. Kuratibu miradi ya Wahisani mkoani
  8. Kumshauri Katibu Tawala wa Mkoa juu ya masuala ya mashirika ya Umma, mashirika yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi
  9. Kuratibu shughuli za utafiti mkoani
  10. Kuratibu zoezi la Sensa.
  11. Kuziwezesha mamlaka za Serikali za mitaa juu ya utekelezaji wa sheria ya mazingira Na. 2 ya 2004.
  12. Kumshauri Katibu Tawala wa Mkoa na Halmashauri juu ya utekelezaji wa sheria za kazi.
  13. Kuratibu masuala ya Maafa katika mkoa.

     

MIPANGO YA MAENDELEO YA MKOA WA MWANZA 2009/10

 

Upanuzi wa jengo la Utawala

Upanuzi wa Hospitali ya Mkoa-SeKou Toure

Ujenzi wa Ofisi ya mkuu wa wilaya ya yamagana

Uratibu wa Mipango ya Kuboresha Kilimo-ASDP

Uratibu wa Mipango ya Kilimo -DASIP

Mfumo shirikishi wa Jamii-Participatory Appraissal

Mfuko wa mkuu wa Mkoa Kuchangia Miradi ya Maendeleo

  •  
     

    MIPANGO

    Mipango katika  Tanzania inatekelezwa katika ngazi mbalimbali.
    Katika ngazi ya Taifa  kuna agenda za Muda mrefu (Framework) za kitaifa .Hii ni mikakati ambayo imeandaliwa kwa ajili ya maamuzi ya jumla  kama dira ya Pamoja  kwa siku zijazo.Mifano ya mikakati hii ya kiataifa ni VISION 2025,Mpango Mkakati wa Muda wa Kati (Medium Term Plan) na Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania (MKUKUTA ). Chini ya  ngazi taifa kuna Mipango ya Kitaasisi.abla ya mkukuta kulikuwa na mipago mbalimbali hivyo MKUKUTA  ni jitihada mbadala ya Tanzania katika kupunguza umasikini,mikakati ya awali ilikuwa na dhana finyu ya umaskini ambapo MKUKUTA umejikita Katika imani kuwa umasikini ni suala mtambuka na pana  na suluhisho lake ni mikakati yenye mawanda mapana ,hivyo ni suluhisho limejikita katika Nyanja tatu (3) ambazo ni;

    1. Kukuza kipato na kupunguza maskini.
    2. Kuboresha Maisha na Ustawi wa jamii.
    3. Utawala Bora na Uwajibikaji.

    MKUKUTA kama zana ya upangaji ina malego makuu mawili;

    1. Unafanya kazi kama muongozo wa kufikiwa kwa matokeo ya kukua kwa kipato na kupunguza Umaskini pia kama muogozo wa hatua za kuchukuliwa kama vipau mbele vya kukuza kipato na kupunguza umaskini katika serikali,asasi za kiraia  na sekta binafsi.
    2. Unaelekeza  kuelekeza fedha za umma kweye hivyo vipaumbele.

    Mfumo wa Menejimenti ya Ufanisi (Performance Management System- (PMS) kupitia Dhana ya Kuboresha Ufanisi (Performance Improvement Model)-PIM,inayosimamiwa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma-OR-MUU inayokusudia  kuboresha Ufanisi wa Wizara,Idara na wakala wa serikali (MDAs),Sekretarieti(RSs) za mikoa na Mamlaka za serikali za Mitaa (LGAs ). Kupitia utaratibu huu serikali imeamua  kuwa Wizara,Idara na wakala wa serikali (MDAs),Sekretarieti(RSs) za mikoa na Mamlaka za serikali za Mitaa (LGAs ) zote kuwa na Mipango mikakati (Strategic Plans/Institutional Plans) inayo onyesha/bainisha mwelekeo wa kufikia malengo na majukumu yake katika muda wa kati,vile vile hii ina tekeleza malengo ya maendeleo ya Milenia,Dira ya Taifa ya Maendeleo(Vision 2025) na nyanja zingine muhimu. Mipango hii inabainisha ni matokeo gani Taasisi inatarajia kufanya,nini ifanye na kwa sababu zipi,Mpango mkakati ni mpana zaidi ya MKUKUTA. Mpango mkakati (Strategic Plan-SP) wa taasisi yeyote una sifa kuu zifuatazo:

    1. Uchambuzi wa hali halisi ilivyo (Situational analysis) hii huuangalia asili ya taasisis,majukumu na kazi  za taasisi ,Uchambuzi wa Wadau na Tathmini ya ndani na nje ya Taasisi kwa kutumia utaratibu wa  “SWOC/SAOC”
    2. Dira ya Taasisi.
    3. Mwelekeo
    4. Malengo
    5. Mikakati (Strategies)
    6. Shabaha (Targets)
    7. Vigezo vya kupima Ufanisi (Performance Indicators)

    Mpango huu wa mipango unawapa nguvu wananchi katika kufanya maamuzi  katika Nyanja  mbalimbali za maendeleo.Katika ngazi za serikali za mitaa  mchakato wa mipango unafuata methodolojia ya muongozo wa Fursa na vikwazo vya maendeleo “Opportunities and Obstacles to Development-(O&OD)”.Ni mpango shirikishi jamii wa Upangaji mipango wenye sifa zifuatazo;

    • Ni methodolojia inayoanzia chini kuja juu(bottom up methodology)
    • Inaanza na Fursa badala ya vikwazo ili kukuza ari kuanza na fursa zilizopo katika eneo husika na kuamusha kujitegemea na kumiliki maedeleo  kwa jamii yenyewe.
    • Inajenga daraja kati ya Serikali za mitaa/Vijiji na Halmashauri zenyewe( LGAs).
    • Inafanya kazi ndani ya muundo wa Halmashauri( LGAs)na kuzingatia Mipango ya jumla ya kitaifa.
    • Inawawezesha kuandaa mipango yao kwa kutumia dira ya maedeleo ya Taifa ya 2025.
    • Ina shirikisha sekta nyingi (multi-sectoral)
    • Inajega uwazi na uwajibikaji (Transparency and accountability)
    • Inazi wajibisha Serikali kuu na za mitaa kukidhi/kutatua mahitaji wa jamiiIt helps
    • Serikali za mitaa zinaratibu shughuli za wadau wa maendeleo.
    • Ina jenga uwezo wa jamii kutatua masuala ya mtambuka.( cross- cutting issues)
    • Inakuza mahusianao kati ya sekretarieti ya mkoa a serikali za mitaa kupitia kujenga uwezo.
     
    VIPAU MBELE VYA MKOA WA MWANZA

     

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Upanuzi wa Jengo la Regional Block

    1,500,000,000

    2.

    Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nyamagana

    800,000,000

    3.

    Ununuzi wa Boat 2 Ukerewe na Sengerema

    600,000,000

    4.

    Ujenzi wa ofisi za Makatibu Tarafa Tshs.40,000,000

    5,320,000,000

     

    Halmashauri ya JIJI LA MWANZA

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Ujenzi wa vyumba 180 vya  madarasa ya shule za sekondari

    1,500,000,000

    2.

    Uendelezaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Butimba

    750,000,000

    3.

    Upanuzi wa mto mirongo (kujenga kuta km.6)

    6,500,000,000

    4.

    Ujenzi wa barabara ya kijiji – Kiloleli (km.3) kwa kiwango cha lami

    2,500,000,000

    5.

    Ujenzi wa barabara inayoelekea Chuo cha Ualimu cha Butimba (km. 2.5) kwa kiwango cha lami

    2,000,000,000

    6.

    Ujenzi (Upgrading) wa Barabara zinazoelekea shule mpya za sekondari

    500,000,000

    7.

    Ujenzi wa Agricultural Resource Centre ya Sangabuye

    30,000,000

     

    Uanzishaji wa Benki ya wananchi  ya Mwanza (Mwanza Communicy Bank)

    250,000,000

    8.

    Uanzishaji wa ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya ya Ilemela

    1,000,000,000

    9.

    Ujenzi wa josho la fumagila

    35,000,000

    10.

    Ulipaji wa fidia ya Ardhi na mimea

    800,000,000

    11.

    Ujenzi wa miradi ya Maji ya Igombe, Kayenze na Buhongwa

       1,500,000,000

    12.

    Ununuzi wa skip loaders 2 kwa ajili ya kubeba taka ngumu

    380,000,000

     

    Jumla

    17,745,000,000

     

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Uejnzi wa vyumba 28 vya madarasa

    340,2000,000

    2.

    Ukamilishaji wa nyumba za walimu 15

    288,000,000

    3.

    Ujenzi wa maabara 1

    36,000,000

    4.

    Ukarabati wa vituo 2 vya Afya

    104,000,000

    5.

    Ukarabari wa Zahanati  12

    224,000,000

    6.

    Ujenzi wa Zahanati 5

    105,000,000

    7.

    Ujenzi wa visima virefu vya maji

    25,000,000

     

    Ujenzi wa matanki ya kuvunia maji ya mvua (Sekondari)

    54,000,000

    8.

    Uimarishaji wa mradi wa Maji Mjini (Ngudu)

    50,000,000

    9.

    Ujenzi wa nyumba 4 za watumishi

    220,000,000

    10.

    Ukarabati wa jengo (Boma) la Halmashauri

    28,000,000

    11.

    Uimarishaji wa km za barabara

    233,428,000

    12.

    Ujenzi wa madaraja

    80,500,000

     

    Jumla

    1,788,528,000

     

     

    HALMASHAURI YA WILAYA YA UKEREWE

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Kukarabati jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya awamu ya pili

    320,000,000

    2.

    Kujenga nyumba 5 za watumishi

    190,000,000

    3.

    Kujenga vyumba vya madarasa katika shule za msingi 60

    186,000,000

    4.

    Kujenga nyumba za walimu 10 shule za msingi

    45,000,000

    5.

    HIV/AIDS

    145,000,000

    6.

    Kununua boti 1 iendayo kwa kasi

    130,000,000

    7.

    Kununua gari la taka ngumu

    110,000,000

    8.

    Kununua gari (lori) kwa ajili ya Idara ya Elimu

    110,000,000

    9.

    Kuendesha mpango wa O & OD

    45,000,000

    10.

    Uendelezaji kilimo (District Agriculture Development Support)

    135,000,000

    11.

    Kujenga bwawa la maji machafu (sewerage lagoon)

    150,000,000

    12.

    Uimarishaji wa km za barabaraUkarabati wa zahanati/vituo vya afya

    57,000,000

     

    Jumla

    1,623,000,000

     

     

    HALMASHAURI YA WILAYA MISUNGWI

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Mradi wa maji toka ziwa Victoria

    2,000,000,000

    2.

    Kujenga nyumba za watumishi 10 (wakuu wa idara)

    500,000,000

    3.

    Ujenzi wa ukumbi wa Halmashauri

    100,000,000

    4.

    Ununuzi wa gari kwa ajili ya uratibu wa miradi

    100,000,000

    5.

    Gharama za upimaji viwanja

    50,000,000

    6.

    Mkopo kwa ajili ya fidia ya viwanja

    185,000,000

    7.

    Ujenzi wa hospitali ya Wilaya

    1,500,000,000

    8.

    Ununuzi wa ambulance na gari moja (kila moja 100,000,000)

    200,000,000

    9.

    Kujenga madarasa 82 ya sekondari za kata

    574,000,000

    10.

    Kujenga maabara 20

    540,000,000

    11.

    Kujenga nyumba za walimu 60

    840,000,000

     

    Jumla

    6,589,000,000

     

     

    HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    Na.

    Jina la mradi

    Gharama (Tshs)

    1.

    Ujenzi wa vyumba 10  vya madarasa ya ‘A’ level

    8,750,0000

    2.

    Ujenzi wa maabara 3 za shule za sekondari

    60,884,344

    3.

    Ujenzi wa vyumba 30 vya madarasa ya sekondari

    382,352,335

    4.

    Ukamilishaji wa nyumba za walimu wa sekondari

    339,001,254

    5.

    Ukamilishaji wa madarasa 6  ya shule za msingi

    25,530,000

    6.

    Ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa /Msingi

    8,400,000

    7.

    Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya

    78,750,000

    8.

    Ukamilishaji OPD Luchili na Karumo

    14,700,000

    9.

    Ukamilishaji nyumba za watumishi

    32,655,000

    10.

    Ukarabati wa zahanati na vituo vya Afya

    685,461,063

    11.

    Matengenezo ya kawaida

    183,810,000

    12.

    Matengenezo ya sehemu korofi

    123,604,800

    13.

    Matengenezo ya muda maalum

    226,000,000

    14.

    Madaraja na makalvati

    63,975,2000

    15.

    Uendelezaji kilimo cha pamba

    12,159,910

    16.

    Uzuiaji magonjwa na  visumbufu vya mimea

    4,800,000

    17.

    Uendelezaji ushirika

    6,000,000

    18.

    Uendelezaji Kilimo cha Wafanyakazi

    12,099,395

    19.

    Uzuiaji magonjwa  ya wanyama

    15,356,173

    20.

    Kupambana na kichaa cha mbwa

    4,800,045

    21.

    Ununuzi wa gari kwa shughuli za ugani

    70,779,072

    22.

    Uendelezaji kilimo cha umwagiliaji

    42,918,249

    23.

    Uendelezaji mazao mchanganyiko ya Biashara

    32,091,925

    24.

    Uimarishaji wa miundombinu ya mifugo

    44,400,000

    25.

    Miundombinu ya DASIP

    293,155,000

    26.

    Ukarabati wa miundombinu ya Maji

    631,000,000

    27.

    Ukarabati wa Ofisi ya Maji

    52,000,000

     

    Jumla

    3,505,433,765

     

     
     
     
    [ Mipango ] [ Nyumbani ] au
    Rudi juu
     
         
    © 2009 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa S.L.P 119 Mwanza, Simu:028-2501037/2500366,Fax: 0282501057;Email:info@mwanza.go.tz