KILIMO |
|
| |
| Dr.Sarakikya |
| Katibu Tawala Msaidizi |
| Huduma za Uchumi |
|
aas4@mwanza.go.tz |
| Utangulizi |
| |
Mkoa wa Mwanza unalo eneo linalofaa kwa kilimo linalokadiriwa kuwa hekta 1,142,685 sawa na asilimia 32 ya eneo la mkoa na asilimia 57 ya eneo la nchi kavu. Eneo linalotumika kwa kilimo ni hekta 740,000 sawa na asilimia 64.7 ya eneo la kilimo. Wastani wa eneo la ardhi kwa kaya ni hekta 3.5 na wastani wa eneo la kilimo kwa kaya ni hekta 2. Majedwali haya hapa chini yanatuonyesha hali halisi ya idadi ya watu, kaya, na eneo la ardhi kwa matumizi ya kilimo.
|
| |
HALI YA KILIMO:
Kutokana na sensa ya watu ya mwaka 2002 ambapo mkoa ulikuwa na watu 2,942,248, mwaka huu (2007) mkoa unakadiriwa kuwa na watu 3,443,998. Idadi hii ya watu mahitaji yao ya chakula aina ya wanga ni tani 868,700. Hivyo malengo ya mkoa ya uzalishaji wa chakula yanatakiwa yasiwe chini ya kiwango hiki ili tuweze kujitosheleza kwa chakula.
Hali ya kilimo msimu 2006/2007:Msimu wa kilimo 2006/2007 mkoa ulilenga kulima hekta 603,470 za mazao ya chakula zenye kutarajia kutoa mavuno ya tani 995,652. Zao la biashara (pamba) mkoa ulilenga kulima hekta 140,873 zenye kutarajia mavuno ya tani 211,309 |
|
Hadi shughuli za kilimo zinamalizika, eneo la hekta 557,072 za mazao ya chakula zilikuwa zimelimwa. Hii ni sawa na asilimia 92 ya lengo. Eneo hili linakadiriwa kutoa mavuno ya tani 921,881 yaani tani 872,957 za chakula aina ya wanga na tani 39,924 za chakula aina ya mikunde (protin)Zao la biashara (pamba) hadi msimu wa kilimo cha zao hili unamalizika, eneo la hekta 99,340 lilikuwa limelimwa. Hii ni sawa na asilimia 70 ya lengo. Eneo hili linakadiriwa kutoa mavuno ya tani 40,829.Changamoto inayoukabili mkoa ni kuongeza uzalishaji kwa eneo |
.  |
UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA
Msimu wa ununuzi wa zao la pamba ulifunguliwa rasmi tarehe 25.06.2007 ambapo mkoani Mwanza waombaji 26 walikubaliwa kununua pamba kutoka kwa wakulima. Wakati msimu unaanza bei ya kununulia pamba ilikuwa Tshs.350 kwa kilo lakini bei ilipanda hadi kufikia Tshs.450 – 550 kwa kilo kutegemeana na mnunuzi na ushindani. Bei hii haijawahi kufikiwa tangu kilimo cha zao hili kianze mkoani. Bei hii kubwa inatokana na uzalishaji mdogo wa zao hili msimu huu. Hadi tarehe 31.08.2007 ikiwa ni wiki ya 10 tangu msimu wa ununuzi uanze kilo 35,951,224 zilikuwa zimeishanunuliwa kutoka kwa wakulima zenye thamani ya Tshs. Billioni 16.1.
|
|
Agizo la kuongeza uzalishaji wa zao la Pamba kwa ekari:
Tarehe 15/05/2006, selikari ilitoa agizo la kuongeza uzalishaji wa zao la pamba kutoka kilo 300 hadi 1000 kwa ekari
Kufuatia agizo hilo mkoa uliandaa mkakati wa kutekeleza agizo hilo. Baadhi ya mikakati hiyo ilikuwa:
- Kuongeza matumizi ya mbolea ya samadi ambapo tani 295,870 zilisombwa na kupelekwa mashambani ikilinganishwa na tani 113,200 zilizopelekwa msimu uliopita.
- Kuongeza matumizi ya mbolea za viwandani ambapo tani 555 za mbolea ya ruzuku zilinunuliwa ikilinganishwa na tani 315 msimu uliopita.
Mvua nyingi iliyonyesha iliathiri upandaji palizi, na ustawi wa zao hili. Hata hivyo tathmini iliyofanyika inaonyesha kuwa wastani wa uzalishaji kimkoa msimu huu kilimo ni kilo 411 kwa ekari.
Mkakati wa kuboresha zao la pamba ulioandaliwa na mkoa utasimamiwa kikamilifu ili uweze kutekelezwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji hadi kufikia kilo 1000 kwa ekari ifikapo 2010.
|
|
|
UPATIKANAJI WA PEMBEJEO Pembejeo za kilimo muhimu mkoani yaani mbolea, madawa na mbegu bora zinaendelea kupatikana kwa mawakala binafsi ambao huleta kufuatana na mahitaji na ununuzi kutoka kwa wakulima. Hata hivyo pembejeo nyingi zinapatikana makao makuu ya mkoa na wilaya, na chache katika maeneo ya vijijini. Changamoto iliyopo ni kuendelea kuhamasisha wakulima kutumia pembejeo ili kuongeza tija katika kilimo. Vilevile kuhamasisha wafanya biashara wenye uwezo kifedha maeneo ya vijijini na vyama vya kuweka na kukopa kuwa mawakala wa pembejeo.
Mkoa unao mawakala wa pembejeo wapato 79. Idadi hii ni ndogo ikilinganishwa na idadi ya vijiji ikilinganishwa na maduka ya madawa ya binadamu ambayo idadi yake ni zaidi ya 700.
Mbolea ya ruzuku:
Mkoa ulipangiwa tani 650 za mbolea ya ruzuku. Hadi mwisho wa kipindi cha ruzuku tani 555 zilikuwa zimenunuliwa na mawakala walioteuliwa na wilaya. Jedwali lifuatalo linaonyesha usambazaji wa mbolea na madawa ya pamba kwa misimu ya 2006/2007. |
| |
| KILIMO CHA UMWAGILIAJI: |
| |
Kutokana na kuwepo kwa maji ya kutosha yanayotokana na ziwa Victoria, mito na maeneo tambarare, mkoa unalo eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji linalokadiriwa kufikia hekta 30,023Pamoja na mkoa kuwa na eneo kubwa linalofaa kwa kilimo hiki, eneo la hekta 2,468 sawa na asilimia 8.2 ndilo limeendelezwa kwa kilimo cha umwagiliaji. Wananchi wanahimizwa kutumia kilimo hiki badala ya kutegemea sana mvua. |
|
MATUMIZI YA ZANA ZA KILIMO:
Lengo la matumizi ya zana za kilimo ni kurahisisha na kuharakisha shughuli za kilimo kwa kutumia zana za kilimo kama vile trekta, jembe la kukokotwa na ng’ombe.
Hadi sasa mkoa umekadiriwa kuwa na matreka 190 na plau za kukokotwa na ng’ombe zipatazo 30,282. Asilimia 2.8 ya wakulima hutumia trekta, asilimia 32.3 hutumia plau na asilimia 64.9 bado hutumia jembe la mkono. Jedwali lifuatalo hapa chini linaonyesha matumizi ya zana ya kilimo kiwilaya |
HUDUMA ZA UGANI:
Huduma za ugani zinafanywa na watumishi 282. Idadi hii ni ndogo ikilinganishwa na eneo la mkoa lenye kata 175 na vijiji 706.
Kutokana na hali hii mkoa umekuwa ukizishauri Halmashauri kufanya yafuatayo ili kukabiliana na upungufu huu.
1.Kujadiliana na wadau wengine wa sekta ya kilimo i.e. wanunuzi wa zao la pamba ili waweze kuajiri maafisa ugani kwa zao la pamba na kuwapatia vitendea kazi.
2.
Ushauri wa maafisa ugani kwa wakulima ufanyike kwa vikundi zaidi kuliko kutembelea mkulima mmoja mmoja. |
UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO (ASDS):
Mkakati wa kuendeleza sekta ya kilimo unatekelezwa kupitia programu ya kuendeleza kilimo (Agricultural Sector Development Programme). Ngazi ya wilaya mkakati huu unatekelezwa kupitia mipango ya maendeleo ya kilimo wilayani (District Agricultural Development Plans – DADPS)
Mwaka 2006/2007 miradi 44 ya sekta ya kilimo, mifugo na ushirika yenye thamani ya Tshs.281,000,000 ilitekelezwa.
Aidha mwaka 2007/2008 miradi ya kilimo, mifugo na ushirika ipatayo 138 yenye thamani ya Tshs. Billion 4.5 imepangwa kutekelezwa msimu huu.
|
|
| |
|
|
|
| |
| Mikakati ya kuendeleza mifugo: |
|
kutokana na changamoto zinazotukabili katika sekta hii hususani miundo mbinu ya sekta ambayo haitoshelezi, juhudi na mikakati ya mkoa katika kuendeleza mifugo ni :-
1.Kutoa ushauri kwa serikali za Vijiji kufanya jitihada za kulinda maeneo ya malisho yaliyopo ili yasiendelee kuvamiwa kwa shughuli za kilimo.
2.Kutoa ushauri kwa wafugaji kutunza masalia mbalimbali baada ya mavuno ili yatumike kulishia mifugo yao.
3.Kutoa ushauri wa kupanda malisho bora (majani na jamii ya mikunde).
4.Kuwaelimisha wafugaji umuhimu wa kuogesha mifugo yao kila mara kuzuia magonjwa yaenezwayo na kupe.
5.Kuwaelimisha wafugaji ili waweze kuyakarabati majosho na malambo ya maji katika maeneo yao.
6.Kutoa elimu kwa wafugaji kuwa na ng’ombe chotara wanaotoa maziwa mengi kwa kutumia njia ya kuzalisha chotara kwa kutumia madume bora au uhamilishaji (artificial insemination).
7.Kushauri wafugaji juu ya umuhimu wa chanjo mbalimbali kwa magonjwa ya mifugo yasiyokuwa na tiba kama vile mdondo, ugonjwa wa miguu na midomo na kichaa cha mbwa n.k.
8.Kushauri wafugaji kubadili ulishaji wa mifugo yao kwenye maeneo yenye uhaba wa ardhi kama Ukerewe na Mijini kwa kulishia mifugo (ng’ombe na mbuzi wa maziwa) ndani (Zero –grazing).
9.Kutoa elimu ya muda wa kuchunga mifugo usiopungua saa nane kila siku.
10.Kutoa elimu juu ya ufugaji wa mbuzi wa maziwa kwa madhumuni ya kutoa maziwa hayo kwa jamii hasa kwa watoto na wazee.
11.Kuendeleza ufugaji wa nguruwe kwa ajili ya kuinua kipato cha wananchi.
12.Kuhamasisha na kutoa elimu kwa wafugaji ili waweze kuunda kamati za kutatua matatizo yao kama vile kamati za majosho, kuunda umoja wa wafugaji kuanzia ngazi ya Kijiji hadi Wilaya.
13.Kutoa elimu kwa wafugaji ili waweze kujenga mabanda bora ya ndama, mbuzi, Kondoo, kuku, nguruwe kwa madhumuni ya kuzuia magonjwa yaletwayo na baridi kama kichomi (pneumonia).
14.Kuwaelimisha wafugaji kuwa na mazizi safi na kuhakikisha ya kwamba samadi inaondolewa kwenye mazizi na kusambaza mashambani, ili kuzuia magonjwa ya kwato (foot-rot). |
| |
|