Kimsing , bajaeti ni mchakato wa kugawa raslimali kwa namna nzuri zaidi ya mpago.Kwa maneno mengine bajeti ni namna ya kuufanya mpango ufanye kazi i.e. Ni mchakato wa kubadilisha mipango kuwa katika mfumo wa fedha.Ni kazi endelevu inayojibu swali nii kifanyike ili kukamilisha mpango kazi kwa ufanisi zaidi.
Mpango wa matumizi wa muda wa Kati (MTEF) uliaza kama jitihada za bajeti ya oparasheni maalumu lakini kadiri siku zinavyokwenda imekuwa ikitumika kama zana ya kufanyia mipango(planning tool). MTEF ulibuniwa kwa ajili ya kuleta ufanisi kwenye kugawa raslimali na uko chini ya wizara ya Fedha na Uchumi.Ni lazima kwa Wizara,Idara,Wakala(MDAs) na Mamlaka za serikali za mitaa(LGAs)It is an obligation that MDAs, RSs and LGAs kuandaa bajeti zake kwa kufuata utaratibu wa MTEFU ambao kimsingi umegawanyika katika sehemu kuu nne(4) ambazo ni : - Malengo (Objectives)
- Shabaha (Targets)
- Activities and
- Vitendea kazi (Inputs).
MTEF umekuwa ni injini/muhimili wa mchakato wa upangaji mipango serikalini. Kupitia utaratibu huu raslimali zinagawanywa na mipango inatekelezwa.
MTEF ni vipaumbele vya miaka mitatu vya makisio kwa pamoja (matumizi ya kawaida a maendeleo,vyanzo vya serikali na wadau wa maendeleo) ambao umejikita kwenye viashiria vya ufanisi katika mpango mkakati(strategic plan).Ni mchanganyiko wa mpango unaotekelezwa(rolling plan) na bajeti ijayo (forward budget (RPFB)) na Bajeti ya ufanisi(performance budget).
Malengo mahususi ya MTEF ni:
- Kuifanya bajeti itabirike kwa kuchochea ukusanyaji wa vyanzo vya mapato vya ndani ,kuweka pamoja fedha za nje kuhakikisha uwiano ili kuendana na mgawanyo unaokubalika unaozingatia vipaumbele.
- Kuwezesha kujitoshereza kibajeti kwa kuhakikisha kuwa gharama za utekelezaji wa shughuli zina zinabebeka kwa kutumia raslimali zilizopo na za baadaye.
- Kupunguza utegemezi wa bajeti kutoka kwa wahisani wa Miradi/Programu kuwezesha ugawaji wa raslimali kwenye uwekezaji na matumizi megine.
- Kuimarisha bajeti yenye kuzingatiamatokeo(output oriented budget) ambayo inalenga katika kuboreshautoaji wa huduma bora.
Uwasilishaji wa Mipango na Bajeti:
- Mipango na bajeti za Vijiji/kata katika Timu ya Menejimenti ya Halmashauri( Council Management Team) kwa ajili ya uchambuzi, vipaumbele na kuwekwa pamoja( consolidation).
- Mkurugenzi wa Halmashauri (Council Director) kuwasilisha mipango na bajeti kwenye Timu ya Menejimenti ya Mkoa (Regional Management Forum) kwa ajili ya ushauri wa kiataalamu.
- Mipango na Bajeti kuwasilishwa kwenye Kamati ya Ushauri ya Wilaya(District Consultative Committee)
- Mipango na Bajeti kuwasilishwa kwenye Kamati ya Ushauri ya Mkoa(Regional Consultative Committee)
- Mipango inarudishwa kwenye kamati ya Fedha ya Halmashauri husika.
- Mipangoa na Bajeti kuwasilishwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani( Full Councils) husika kwa ajiri ya kupitishwa
- Mipango na Bajeti kuwasilishwa kwenye Sekretariati ya mkoa husika kwa majumuisho (consolidation).
- Mipango na Bajeti kuwasilishwa Wizara ya Fedha (MOFEA) na Wizara ya TAMISEMI(PMORALG) kwa uchambuzi.
- Wizara ya Fedaha na Uchumi(MOFEA) huwasilisha Mipango na Bajeti kwenye Kamati ya kitaalamu ya wizara (Inter Ministerial Technical Committee) na Baraza la Mawaziri kwa uthibitisho.
- TAMISEMI na RS kuwasilisha Mipango na Bajeti Kwenye Kamati ya Bunge ya Kisekta .
- Mipango na Bajeti huwasilishwa Bungeni kwa uthibitisho wa mwisho.
|