JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
 
     
DIRA NA MWELEKEO WA MKOA
 
[ Dira Mwelekeo] [ Nyumbani ] au
 
DIRA (VISION)
 

Dira (Vision) ya Maendeleo ya Mkoa wa Mwanza ni kuhakikisha Mkoa unakuwa taasisi yenye uadilifu katika kutekeleza majukumu yake, hususani kuzisaidia Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kwa kuzijengea uwezo ili ziweze kutoa huduma bora za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

 
 
 
 
Mwelekeo (Mission)
 

Mwelekeo wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ni pamoja na:
(a) Kujenga uwezo wa Serikali za Mitaa ili ziweze kutoa huduma bora za kiuchumi na kijamii kwa wananchi ili ziweze kuhimili changamoto za maendeleo katika maeneo yao

(b) Kuendeleza raslimali watu katika Sekretariati ya Mkoa ili iweze kujijengea uwezo Serikali za Mitaa.
 Kwanza napenda kuelezea kuwa mafanikio ya utekelezaji wa mpango wa muda wa kati wa 2008/2009  - 2010/2011 utaendelea kuzingatia sera ya serikali kuhusu upelekaji wa madaraka kwa wananchi kwa kuzingatia majukumu yaliyopewa mkoa katika kuwaletea wananchi maendeleo. Majukumu haya yamegawanyika katika sehemu mbili.  Yapo majukumu ya kisera na majukumu ya kiutendaji

 

 
Mandate (Majukumu)

Majukumu ya Sekretarieti ya mkoa ni kutafsiri sera,kujijengea uwezo na kuzisaidia serikali za mitaa kutekeleza majukumu yake ya kijamii na kiuchumi na huduma za maendeleo na kuhakikisha kuwa kua amani a utulivu katika mkoa.

Wajibu na Kazi

Wajibu na kazi za sekreatarieti ya mkoa ni mengi na yamekasmiwa kwa kila Klasta na Kitengo(section and Unit) .Kwa ujumla jukumu kubwa linalenga kumsaidia mkuu wa mkoa kama ifuatavyo:-
1.Kutekeleza kazi za serikali ndani ya mkoa.
2.Kusimamia utawala wa sheria mkoani.
3.Kutoa mwelekeo wa jitihada katika kutekeleza sera mbalimbali mkoani.
4.Kuzishauri a kuzisaidia Serikali za mitaa kutekeleza mipango yake kwa lengo la kuleta maendeleo na kuodoa umaskini.
5.Kutekeleza kazi namajukumu mengine ya RS ya kisheria.
Majukumu ya kimaendeleo yanajumuisha usimamizi na tathmini,uwezo wa kiutawala wa kutekeleza kutoa huduma.Tathmini ya utoaji huduma inajikita kwenye kufikiwa kwa malengo na matokeo ya malengo hayo katika jamii.
Majukumu ya kiutawala yana sehemu kuu tatu:-
1.Kulinda amani na utulivu katika mkoa ili wananchi watekeleze majukumu yao.
2.Kuziwezesha na Kuzisaidia Serikali za mitaa katika mkoa kutekeleza majukumu yake kwa kuzijengea mazigira bora ya kutekeleza majukumu na wajibu wake.
3.Kuiwakilisha serikali kuu katika mkoa.

 

MAJUKUMU YA MKOA

 
 
 

Majukumu ya kisera ya Mkoa ni pamoja na :

  • Kuhakikisha kuwa kuna hali ya amani na utulivu Mkoani.
  • Kujenga na kuimarisha demokrasia na utawala bora.
  • Kusimamia hifadhi ya mazingira na
  • Kusimamia vita dhidi ya UKIMWI na Rushwa.
 
 
. Majukumu ya kiutendaji ambayo utekelezaji wake ni wa siku zote ni pamoja na:-
 

. Majukumu ya kiutendaji ambayo utekelezaji wake ni wa siku zote ni pamoja na:-
1.Kuratibu na kusimamia Halmashauri za Wilaya na Mji ili ziweze kutekeleza wajibu na majukumu yake kwa wananchi.
2.Kusimamia sera za maendeleo vijijini na mijini.
3.Kusimamia Mpango wa Uboreshaji wa Serikali za Mitaa mkoani ili uweze kutoa huduma bora.
4.Kuzijengea Serikali za Mitaa uwezo wa kusimamia mapato na matumizi.
5.Kuboresha miundo, hali ya watumishi na mifumo ya kazi ndani ya Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri.
6.Kusimamia Miradi inayotekelezwa chini ya Katibu Tawala Mkoa.
7.Kuratibu utekelezaji wa shughuli za hifadhi ya mazingira katika Serikali za Mitaa.
8.Kutekeleza na kusimamia utekelezaji wa vipaumbele vya mkoa wetu ambavyo ni kilimo cha umwagiliaji, kuimarisha ushirika na hasa vyama vya kuweka na kukopa SACCOSS, programu ya uvutiaji wawekezaji mkoani, usafi wa miji yetu na kuimarisha elimu ya msingi na kujenga shule za sekondari kila kata kufuatana na mahitaji ya kata hizo.
9.Kuhimiza uzalishaji viwandani na mashambani ili kuleta ukuaji wa uchumi kwa maendeleo ya wananchi.
10.Kusimamia maendeleo ya kijamii hususan elimu, afya, maji, kilimo na barabara vijijini
      Ili kutekeleza majukumu haya, mwelekeo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni kuhakikisha  kwamba maamuzi mbalimbali ya Serikali yanayoelekezwa Wilayani pamoja na kwenye
    Serikali za Mitaa yanatekelezwa kikamilifu.  Aidha Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inafanya yafuatayo:-
1. Kufuatilia na kuhakikisha kwamba Mipango ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa inatekelezwa kwa ukamilifu na malengo yake yanafikiwa.
2.Kuhakikisha kwamba Serikali za Mitaa zinaendeshwa kwa misingi ya utawala bora.
3.Kuhakikisha kwamba kunakuwepo uratibu wa sera za Kisekta na programu za maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.
4.Kujenga uwezo wa Sekretarieti ya Mkoa wa kusimamia utekelezaji wa Sera za kisekta na maagizo ya Serikali kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

 

 
     
 
 
[ Dira Mwelekeo ] [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
© 2009 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa S.L.P 119 Mwanza, Simu:028-2501037/2500366,Fax: 0282501057;Email:info@mwanza.go.tz