Majukumu ya Sekretarieti ya mkoa ni kutafsiri sera,kujijengea uwezo na kuzisaidia serikali za mitaa kutekeleza majukumu yake ya kijamii na kiuchumi na huduma za maendeleo na kuhakikisha kuwa kua amani a utulivu katika mkoa.
Wajibu na Kazi
Wajibu na kazi za sekreatarieti ya mkoa ni mengi na yamekasmiwa kwa kila Klasta na Kitengo(section and Unit) .Kwa ujumla jukumu kubwa linalenga kumsaidia mkuu wa mkoa kama ifuatavyo:-
1.Kutekeleza kazi za serikali ndani ya mkoa.
2.Kusimamia utawala wa sheria mkoani.
3.Kutoa mwelekeo wa jitihada katika kutekeleza sera mbalimbali mkoani.
4.Kuzishauri a kuzisaidia Serikali za mitaa kutekeleza mipango yake kwa lengo la kuleta maendeleo na kuodoa umaskini.
5.Kutekeleza kazi namajukumu mengine ya RS ya kisheria.
Majukumu ya kimaendeleo yanajumuisha usimamizi na tathmini,uwezo wa kiutawala wa kutekeleza kutoa huduma.Tathmini ya utoaji huduma inajikita kwenye kufikiwa kwa malengo na matokeo ya malengo hayo katika jamii.
Majukumu ya kiutawala yana sehemu kuu tatu:-
1.Kulinda amani na utulivu katika mkoa ili wananchi watekeleze majukumu yao.
2.Kuziwezesha na Kuzisaidia Serikali za mitaa katika mkoa kutekeleza majukumu yake kwa kuzijengea mazigira bora ya kutekeleza majukumu na wajibu wake.
3.Kuiwakilisha serikali kuu katika mkoa. |