JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
 
 
     
    BIASHARA NA VIWANDA:
 
[ Miradi ] Programu.. [ Nyumbani ] au
 
Biashara

Mkoa una jumla ya wafanyabiashara zaidi ya 7,000 wa jumla na rejareja. Biashara zinazohusika ni kama vifaa vya ujenzi, madawa ya binadamu na mifugo, mafuta aina ya petroli, mafuta ya kula, masonara, wauza nguo mpya na mitumba, wauza nafaka, matunda na kadhalika.

 

Viwanda:
Kwa upande wa viwanda mkoa unavyo viwanda ambavyo vinatoa ajira kama iavyoonyeshwa kwenye jedwari chini:

 

 
 

UWEKEZAJI MKOANI MWANZA

Suala la uwekezaji katika Mkoa wa Mwanza lilianza kupewa kipaumbele katika mkoa wetu kwenye mkutano wa uwekezaji (Investors Forum) uliofanyika hapa Jijini Mwanza tarehe 19 – 20/08/2004. Lengo kubwa la mkutano huu lilikuwa kuutangaza mkoa wetu kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika sekta za kilimo, uvuvi, madini, utalii, viwanda na biashara ambazo zina fursa kubwa ya kupiga vita umaskini kutokana na utajiri mkubwa katika sekta hizi kwa kuwekeza katika sekta hizi. Kutokana na mkutano huo mkoa umeanza kupata wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika sekta hizo. Kutokana na dhima ya mkoa ya kuboresha uwekezaji na biashara katika mkoa, mkoa umekwishaunda Baraza la Biashara la Mkoa. Katika vikao vya Baraza hili suala la ardhi ya akiba (Land bank) kwa ajili ya uwekezaji limejitokeza kuwa tatizo kubwa na hivyo kuwa kikwazo cha uwekezaji. Kutokana na tatizo hilo, Baraza sasa linaandaa kikao ambacho kitakachokuwa na agenda moja tu ya kuzungumzia masuala ya ardhi kwa ujumla wake ili kupata ufumbuzi wa tatizo la ardhi kwa wawekezaji. Katika suala la ardhi mkoa unaamini yapo mambo ambayo yatakuwa ndani ya uwezo wa mkoa kuyatatua na yale ambayo yatakuwa nje ya uwezo wa mkoa yatapelekwa kwa mamlaka husika kupata ufumbuzi na ushauri.

 

Jedwali likionyesha Ajira inatokana na viwanda Mkoa wa Mwanza

 

Aina

Idadi

Ajira ya muda na ya kudumu

(i)

Viwanda vya kusindika samaki

6

2538

(ii)

Viwanda vya vyuma

3

391

(iii)

Kusindika vyakula

3

282

(iv)

Maji/soda

2

692

(v)

Pombe

2

692

(vi)

Pamba

12

401

(vii)

Viwanda vya mafuta ya kula

3

491

(viii)

Viwanda vya nguo

1

1183

(ix)

Viwanda vya magodoro

3

136

(x)

Viwanda vya plastic

2

163

 

Jumla

37

6277

 
 
[ Biashara ] [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
© 2009 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa S.L.P 119 Mwanza, Simu:028-2501037/2500366,Fax: 0282501057;Email:info@mwanza.go.tz