Mkoa wa Mwanza una barabara zenye jumla ya urefu wa km.5,598, katika hizo zimo barabara kuu zenye urefu wa km.397, barabara za mikoa zenye jumla ya km.1,087, barabara za Wilaya km.1,398.7 na km.2,715.4 barabara za vijijini.
Mtandao huu ni muhimu sana kwa wakazi zaidi ya milioni tatu na nusu wa mkoa huu katika kupata huduma mbalimbali za kijamii na unategemewa kuwasaidia wakazi hawa katika kukuza na kuendeleza kilimo cha mazao ya chakula na biashara, kuendesha shughuli za uvuvi, uchimbaji wa madini, utalii na shughuli nyingine za kiuchumi.
|